EWURA Banner
HabariLeo Logo
 
Tafuta:
 
 
 
Habari za Biashara na Uchumi

Biashara kimataifa yainufaisha Tanzania
Imeandikwa na Mwandishi wetu; Tarehe: 24th December 2009 @ 09:20 Imesomwa na watu: 859; Jumla ya maoni: 0


Habari Zaidi:
  • Saidieni ujenzi wa nyumba za walimu, Hakielimu waambiwa
  • Sido wawezesha maonesho Singida
  • TLTC yamwaga 118.2m/- Urambo
  • Baraza lazipiga msasa Saccos
  • Precision Air yazindua ndege nyingine mpya
  • TaCRI yawasaidia wakulima Kilimanjaro
  • Wanawake zingatieni masharti ya mikopo -Mama Salma
  • Vodacom yatoa ofa ya Mwezi Mtukufu
  • PSI yasambaza kondomu za mil. 1.5/- kwa waathirika VVU
  • Wakulima 700,000 wakamilisha mzunguko wa vocha za ruzuku
  • Wazee wilaya ya Morogoro kukopeshwa
  • ‘Umoja wa forodha unakuza uchumi’
  • Mkurabita wawataka wasanii kujiweka rasmi
  • Henan kuimarisha uhusiano na Dar es Salaam
  • Kopeni kuleta maendeleo, KCB yaasa
  • Hits yazindua nembo
  • Zain yatoa futari kwa watoto yatima
  • Kiwanda cha kukata madini chazinduliwa Arusha
  • Wakulima wanufaika na soko la mazao
  • Mabasi ya Kangi Bomba kuendelea na biashara

  • Habari zinazosomwa zaidi:
  • Balaa lingine kwa Chenge
  • Salama: Jasiri aliyetangaza kuishi na virusi vya Ukimwi
  • Dina Marius, mrithi wa Amina Chifupa
  • ‘Housigeli’ anataka kuniharibia ndoa
  • Vatican yamvua jimbo Askofu
  • Kikwete achekecha wakuu wa wilaya
  • Waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano waongezeka kwa 22%
  • Interpol yatumika kusaka wenye zeutamu
  • Orijino Komedi, Jay Dee waitwa Iringa
  • JK apigilia msumari wa mwisho Dowans
  • TANZANIA imefaidika katika biashara ya kimataifa, lakini kuna athari ndogo katika utalii na madini kutokana na mtikisiko wa kiuchumi ulioikumba dunia.

    Kwa mujibu wa taarifa za utafiti uliofanywa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT),Tanzania imefaidika na mtikisiko huo wa kiuchumi kwa biashara ya kimataifa kupanda kutokana na kuporomoka kwa bei ya bidhaa katika soko la kimataifa.

    Takwimu za BoT ilizozitoa hivi karibuni pia zimeonesha kuwa mtikisiko huo wa kiuchumi umeleta madhara madogo kwenye utalii na sekta ya madini.

    Bot imesema, hadi Septemba mwaka huu, mapato yatokanayo na kusafirisha bidhaa nje yamepanda kwa asilimia 3.2 ikilinganishwa na muda kama huo kwa mwaka jana.

    Wakati mapato hayo yakiwa yamepanda kutoka Dola za Marekani bilioni 4.5 hadi dola bilioni 4.6, mapato yatokanayo na kuingiza bidhaa nchini yameshuka na kufikia Dola za Marekani bilioni 7.5 kutoka dola bilioni 7.8 katika kipindi hicho kwa mwaka jana.

    Mizania ya biashara ya nchi kati ya mauzo ya nje na bidhaa zinazoingizwa nchini hadi kufikia Septemba mwaka huu, ilipungua kufikia Dola za Marekani bilioni 2.06 kutoka dola za kimarekani bilioni 2.95 kwa mwaka jana katika kipindi kama hicho.

    BoT pia ilieleza kuwa gharama za kuingiza mafuta kutoka nje zilipungua kwa asilimia 24.4 kufikia Dola za Marekani bilioni 1.3 katika mwaka huu unaoishia Septemba.

    Kwa mujibu wa BOT,hali hiyo inatokana na kuanguka kwa bei ya mafuta katika soko la dunia ingawa kiwango cha mafuta kilichoingizwa nchini kiliongezeka kwa tani milioni 2.2 mwaka jana hadi kufikia tani milioni 2.9 mwaka huu.

    Mkuu wa utafiti wa uchumi na sera wa BoT, Joe Massawe alisema, “licha ya kutokea matatizo ya kiuchumi nchini, kushuka kwa bei ya bidhaa katika soko la dunia kumesababisha kushuka kwa gharama za kuagiza bidhaa kutoka nje. Hii pia imepunguza gharama za uzalishaji.”

    Wakati huo huo, Mkuu wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) nchini, David Robinson alisema hali ya kiuchumi nchini ni nzuri wakati huu wa mtikisiko wa kiuchumi duniani na hali hiyo imetokana na Tanzania kutoingiliana sana na uchumi wa kimataifa

     
         
    Email this to a friend   Print this article
    Jumla Maoni (0)
         
     
     
      Tuma Maoni yako
       

    Jina la Kwanza:

    Jina la mwisho:
    Baruapepe: Barua Pepe imekosewa.
    Maoni yako:   Andika Maoni yako tafadhali.Tafadhali andika Maoni yako.
     
     
     
    UCHAMBUZI
    Image

    Magereza fanyieni kazi malalamiko ya wafungwa

    SOMA | HIFADHI
    SAFU
    Image

    Tekuteku za Tefutefu!

    SOMA | HIFADHI
    NYOTA WA WIKI
    Image

    Mtangazaji kajikomboa kwa kuanzisha redio

    SOMA | HIFADHI
    JISAJILI NASI
    Jina la kwanza:
    Jina la Ukoo:
    Baruapepe: A value is required.
     
     
     
    Wasiliana nasi mhariri@habarileo.co.tz, advertising@dailynews.co.tz
    Simu:+255 22 2 127492 au 22 2 116074 au +255 22 2 110595 au 22 2 127493
    HabariLeo © 2009 Haki zote zimehifadhiwa.
    DailyNews Building, Plot 7, Samora Avenue, Box 9033, Dar es Salaam, Tanzania Copyright © 2009 DailyNews Media Group
    Advertisement
    TSN Adveritising