Mgombea urais kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) Dk. Willibrod Slaa akiwahutubia wakazi wa Babati Mjini mkoani Manyara katika mkutano wa kampeni jana. (Na Mpiga Picha Wetu).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 2nd September 2010 @ 23:59
Mgombea wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jakaya
Kikwete akisalimiana na wananchi wa Tukuyu, Mbeya wakati wa
mkutano wa kampeni. (Picha na Freddy Maro).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 1st September 2010 @ 19:18
Wananchi na waumini wa dini ya kiislamu wakiubeba mwili wa marehemu Mufti Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Harith Bin Khelef aliyefariki dunia Alhamisi iliyopita nchini India. Mwili huo ulizikwa jana katika kijiji cha Muyuni wilaya ya Kusini Unguja, Zanzibar.(Picha na Ramadhan Othman).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 1st September 2010 @ 10:50
Baadhi ya wakazi wa Dar es Salaam wakiangalia meli za kivita za Jeshi la Wanamaji la Tanzania, wakati wa maonesho yaliyofanyika eneo la Kigamboni, jana ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 49 ya Jeshi hilo leo. (Picha na Fadhili Akida).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 31st August 2010 @ 19:11
Kamanda wa Chipukizi wa Wilaya ya Masasi, Fatuma Rajab, akimvisha skafu mgombea mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. Mohamed Gharib Bilal, alipokuwa akiingia mpakani mwa Wilaya ya Masasi akitokea Wilaya ya Newala jana. (Na Mpigapicha Wetu).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 31st August 2010 @ 07:52
Wananchi wa Kijiji cha Miembeni Wilaya ya Nachingwea wakimzunguka Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. Gharib Bilal, baada ya kutanda barabarani na kuwaomba viongozi wa msafara kumruhusu kushuka ili wamuone na kusalimiana naye, wakati msafara huo ulipofika mpakani mwa wilaya ya Nanchingwea ukitokea Wilayani Liwale. (Picha na Tiganya Vincent- MAELEZO).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 27th August 2010 @ 20:24
Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF) na Mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahim Lipumba (katikati)akionesha kwa waandishi wa habari ilani ya uchaguzi wa Chama hicho ya mwaka 2010 jana jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mgombea mwenza wa CUF, Juma Duni Haji na kulia ni Mkurugenzi wa Siasa Taifa Mbarala Maharagande. (Picha na Tiganya Vincent, Maelezo).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 26th August 2010 @ 20:21
Mwanafunzi Joel Abdallah anayesoma darasa la tatu katika shule ya msingi Rutozo iliyoko katika kijiji cha Katoro akimsalimia Rais Kikwete muda mfupi juzi kabla ya kupanda helikopta kwenda Muleba, mkoani Kagera kuanza ziara ya siku mbili ya kampeni. (Picha na John Lukuwi).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 25th August 2010 @ 19:35
Maelfu ya wakazi wa mji wa Geita na vitongoji vyake mkoani Mwanza wakimsikiliza kwa makini Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa mkutano wa hadhara juzi mchana (Picha na Freddy Maro)
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 24th August 2010 @ 19:19
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwahutubia wananchi katika kata ya Nyehunge jimbo la Buchosa,wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza Jana.(picha na Freddy Maro)
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 24th August 2010 @ 08:04
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM Rais Jakaya Kikwete akimnadi mgombea ubunge wa chama hicho wa Jimbo la Misungwi Mwanza Charles Kitwanga jana akiwa ni mgombea ubunge wa kwanza kunadiwa na Mwenyekiti huyo wa CCM ambaye kaanza rasmi ziara ya mikoani. (Na Mpigapicha Wetu).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 23rd August 2010 @ 16:19
Sehemu ya umati uliofurika katika viwanja vya Jangwani, Dar es Salaam kushuhudia uzinduzi wa kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa ajili ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 31 mwaka huu.(Picha na Mpiga picha Wetu)
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 22nd August 2010 @ 08:51
Kaimu Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), Mkumbwa Ali (kushoto) akimpa maelezo Balozi wa Zimbabwe nchini Edzai Chimonyo (kulia), kuhusu utendaji wa kampuni katika ofisi za TSN jana. Wengine kutoka kulia ni Ofisa Ubalozi huo, Zvidzai Tahwa, Mhariri wa HABARILEO, Joseph Kulangwa, Meneja Matangazo TSN, Felix Mushi, Mhariri wa Habari HABARILEO Jumapili, Eric Anthony na Mhariri Msaidizi wa Daily News, Gabriel Mgaya. (Na Mpiga Picha Wetu)
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 20th August 2010 @ 19:33
Msafara wa Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi, (CCM), Rais Jakaya Mrisho Kikwete ukipita katika barabara ya Ohio na kuingia kwenye barabara ya Ghana yalipo Makao Makuu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kurejesha fomu Dar es Salaam jana. (Picha na John Lukuwi).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 19th August 2010 @ 19:21
Mshitakiwa wa biashara ya albino Nathan Mtei (wa tatu kushoto) akipelekwa mahakamani huku umati wa watu ukimsindikiza wakiwamo waandishi wa habari na baadhi ya wanachama wa chama cha albino jijini Mwanza kabla ya kuhukumiwa jana. (Picha na Clara Matimo).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 18th August 2010 @ 23:59
Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk.Ali Mohamed Shein, akionesha Fomu za kugombea nafasi hiyo mara baada ya kukabidhiwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC Hatib Mwinchande katika Ofisi ya Tume hiyo Maisara mjini Zanzibar jana.
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 18th August 2010 @ 17:21
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akibonyeza kitufe kuzindua mradi wa Umeme unaotumia gesi ya asili huko Somanga Fungu jana jioni, huku Waziri wa Nishati na madini William Ngeleja(watatu kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Wiliam Mhando(wa nne kushoto) wakiangalia. Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi Said Meck Sadiq.(picha na Freddy Maro)
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 18th August 2010 @ 10:05
Raia wa Kenya Nathan Mtei anayetuhumiwa kumleta nchini mlemavu wa ngozi(albino) Robinson Mkwana Mnyoti (hayupo pichani) ili kumuuza jijini Mwanza. (Picha na Clara Matimo).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 16th August 2010 @ 20:00
Mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale-Mwiru (kushoto), akibadilishana mawazo na katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Chiligati wakati wa mkutano wa Halmashauri Kuu (NEC) wa mchakato wa kupitisha majina ya wagombea wa nafasi za ubunge na udiwani wa chama hicho, mjini Dodoma.Katikati ni Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa.(Picha na Robert Okanda).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 16th August 2010 @ 08:40
Msaada! Mkazi wa Dar es Salaam akiwa amepakiwa kwenye toroli akiwa na mizigo yake kama alivyokutwa barabara ya Bibi Titi, jana. (Picha na Fadhili Akida).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 14th August 2010 @ 20:05
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi( CCM) Taifa, Rais Jakaya Kikwete, akifungua rasmi kikao cha kamati kuu ya CCM Taifa kilichokutana jana katika ukumbi wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa Makao Makuu mjini Dodoma. (Picha na Amour Nassor).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 13th August 2010 @ 19:44
Mwakilishi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika mkutano wa Chadema, Nape Nnauye akijaribishwa vazi la Chadema alipowasili kwenye Mkutano Mkuu Maalumu wa chama hicho Dar es Salaam jana. (Picha na Yusuf Badi).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 12th August 2010 @ 19:12
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Amani Abeid Karume, akikagua gwaride rasmi lililoandaliwa kwa ajili ya kuvunja Baraza la Wawakilishi, Chukwani nje kidogo ya Zanzibar jana. (Picha na Ramadhan Othman wa Ikulu)
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 11th August 2010 @ 22:00
Rais Jakaya Kikwete (katikati) akifungua kitambaa kuzindua ujenzi wa miundombinu ya Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), eneo la Kivukoni, Dar es Salaam jana sambamba na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia, John McIntire. Kushoto ni Waziri wa Miundombinu, Dk. Shukuru Kawambwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi (nyuma ya Rais). (Picha na Fadhili Akida).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 11th August 2010 @ 10:06
Kijana ambaye jina lake halikupatikana mara moja akiwa hoi baada ya kupigwa na wananchi wenye hasira kwa kudaiwa kuiba begi lililokuwa na redio ndani katika eneo la Cape Town, Yombo Buza Temeke Dar es Salaam jana. (Picha na Innocent Mallya).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 9th August 2010 @ 19:20
Mmoja wa wasichana wanaoishi na virusi vya Ukimwi, Neema Raymond (16) akifutwa machozi na waelimishaji rika wa mpango wa kimataifa wa mapambano ya ukimwi wa Dance For Life mara baada ya kutoa historia yake katika Kijiji cha Nzihi, Iringa Vijijini, mwishoni mwa wiki. (Picha na Frank Leonard).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 9th August 2010 @ 09:19
Mgombea Urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), Dkt.Wilbrod Slaa, akizungumza na wakazi wa Dar es Salaam waliofika katika viwanja vya Jangwani kumsikiliza. (Picha na Yusuf Badi)
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 7th August 2010 @ 19:51
Naibu Waziri wa Uchapishaji na Habari wa China, Li Dongdong (wa pili kushoto) akitazama gazeti la HABARILEO wakati alipotembelea ofisi za magazeti ya Daily News, Sunday News, HABARILEO na HABARILEO Jumapili Dar es Salaam jana. Kushoto ni Mpigachapa Mkuu wa Serikali, Kassian Chibogoyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Tanzania Standard Newspapers (TSN) Limited, Wilson Mukama (wa pili kulia) na Naibu Mhariri Mtendaji wa TSN, Mkumbwa Ally (wa kwanza kulia). (Picha na Robert Okanda).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 6th August 2010 @ 21:00
Mgombea Urais kwa Chama Cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba (kulia) na mgombea mwenza wa chama hicho Juma Duni Haji wakionesha fomu za kugombea nafasi hizo baada ya kukabidhiwa na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Rajabu Kiravu (hayupo pichani) jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad. (Picha na Robert Okanda)
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 6th August 2010 @ 09:22
Magari yakipita kwa shida kwenye barabara ya Mkunguni yenye madimbwi eneo la sokoni Kariakoo Dar es Salaam jana. Kuchimbika kwa barabara hiyo kumekuwa ni kero kwa waendesha magari na watembea kwa miguu. (Picha na Fadhili Akida).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 5th August 2010 @ 09:15
Mwenyekiti wa Chama cha Democratic(DP), Christopher Mtikila, akiwa katika gari la wakili wake, Penitho Mandele, baada ya kuachiwa katika Mahakama ya Mwanzo Kariakoo Dar es Salaam jana alipofutiwa shitaka la kifungo cha miezi sita baada ya kulipa deni la Sh.Milioni 9.8 alizokuwa anadaiwa na Pascazia Zelamula Mattete.(Picha na Yusuf Badi).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 3rd August 2010 @ 22:00
Mwenyekiti wa Chama cha DP,Christopher Mtikila,akiwa katika gari la wakili wake,Penitho Mandele,baada ya kuachiwa katika Mahakama ya Mwanzo Kariakoo Dar es Salaam jana alipofutiwa shitaka la kifungo cha miezi sita baada ya kulipa deni la Sh.Milioni 9.8 alizokuwa anadaiwa na Pascazia Zelamula Mattete.(Picha na Yusuf Badi).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 3rd August 2010 @ 18:36
Mgombea Urais kwa Chama Cha Mapinduzi, Jakaya Kikwete(kushoto) pamoja na mgombea mwenza wa chama hicho Dr. Gharib Billal wakionyesha fomu za kugombea nafasi hizo baada ya kukabidhiwa jana kwenye ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC). Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Pius Msekwa(Picha na Fadhili Akida)
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 3rd August 2010 @ 08:57
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Rais Jakaya Kikwete, akipiga kura ya maoni kupendekeza mgombea wa udiwani na ubunge kijijini kwake Msoga, Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani. Anayemshuhudia ni msimamizi wa kituo hicho, Mwajuma Khalfani. (Picha na Juma Kengele).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 2nd August 2010 @ 07:30
Mume wa aliyekuwa mfanyakazi wa TSN, Jennifer Mwela, Innocent Mkindi, akiwa na mtoto wake, Collins mwenye umri wa siku tatu, akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa mkewe nyumbani kwao Mburahati, Dar es Salaam jana. (Picha na Yusuf Badi).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 31st July 2010 @ 21:05
Wasimamizi wa mkutano wa wanachama wa CCM Kata ya Kigogo, Dar es Salaam wakimtoa nje ya ukumbi mmoja wa mwanachama aliyesababisha vurugu kutokana na kumuuliza swali la utatanishi mgombea, Shyrose Bhanji (kushoto) wakati wa mkutano wa kuomba kura wa wagombea Ubunge jimbo la Kinondoni, uliofanyika kwenye kata hiyo jana. (Picha na Fadhili Akida).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 30th July 2010 @ 19:37
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), Wilson Mukama (katikati), akiendesha kikao cha Bodi hiyo kilichofanyika Dar es Salaam jana. (Picha na Yusuf Badi).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 29th July 2010 @ 20:44
Rais Jakaya Mrisho kikwete akizungumza wakati wa mkutano wa 15 wa Wakuu wa nchi za umoja wa Afrika uliofanyika huko Kampala Uganda.
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 28th July 2010 @ 19:15
Msukuma mkokoteni akiwa amesimama katikati ya Barabara akizungumza na simu bila kujali usumbufu aliousababisha kwa madereva wa magari Barabara ya Chang'ombe Dar es Salaam jana. (Picha na Fadhili Akida).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 27th July 2010 @ 20:00
Mkazi wa Manispaa ya Dodoma, ambaye jina lake halikupatikana mara moja, akiwa amebeba zabibu katika eneo la stendi kuu ya mabasi ya mjini Dodoma, akitafuta wateja mwishoni mwa wiki. ( Picha na John Nditi).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 26th July 2010 @ 20:46
Mkazi wa Manispaa ya Dodoma, ambaye jina lake halikupatikana mara moja, akiwa amebeba zabibu katika eneo la stendi kuu ya mabasi ya mjini Dodoma, akitafuta wateja mwishoni mwa wiki. ( Picha na John Nditi).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 26th July 2010 @ 20:45
Mkazi wa Manispaa ya Dodoma, ambaye jina lake halikupatikana mara moja, akiwa amebeba zabibu katika eneo la stendi kuu ya mabasi ya mjini Dodoma, akitafuta wateja mwishoni mwa wiki. ( Picha na John Nditi).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 26th July 2010 @ 20:45
Mkazi wa Manispaa ya Dodoma, ambaye jina lake halikupatikana mara moja, akiwa amebeba zabibu katika eneo la stendi kuu ya mabasi ya mjini Dodoma, akitafuta wateja mwishoni mwa wiki. ( Picha na John Nditi).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 26th July 2010 @ 20:45
Mkazi wa Manispaa ya Dodoma, ambaye jina lake halikupatikana mara moja, akiwa amebeba zabibu katika eneo la stendi kuu ya mabasi ya mjini Dodoma, akitafuta wateja mwishoni mwa wiki. ( Picha na John Nditi).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 26th July 2010 @ 20:45
Mkazi wa Manispaa ya Dodoma, ambaye jina lake halikupatikana mara moja, akiwa amebeba zabibu katika eneo la stendi kuu ya mabasi ya mjini Dodoma, akitafuta wateja mwishoni mwa wiki. ( Picha na John Nditi).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 26th July 2010 @ 20:45
Mkazi wa Manispaa ya Dodoma, ambaye jina lake halikupatikana mara moja, akiwa amebeba zabibu katika eneo la stendi kuu ya mabasi ya mjini Dodoma, akitafuta wateja mwishoni mwa wiki. ( Picha na John Nditi).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 26th July 2010 @ 20:44
Rais Jakaya Kikwete akielekea kwenye mnara wa Mashujaa kuweka mkuki na ngao wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana. (Picha na Fadhili Akida).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 25th July 2010 @ 20:22
Vibarua wa ujenzi wakifanya kazi barabarani hivyo kusababisha foleni ya magari katika mtaa wa Mkunguni, Dar es Salaam.(Picha na Robert Okanda).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 25th July 2010 @ 09:24
Akina mama lishe wa eneo la Feri, Posta wa zamani Jijini Dar es Salaam wakiwa wamebeba madumu ya mafuta aina ya dizeli baada ya kuyachota majini. Inasemekana kuwa kuna meli ilikuwa imetoboka na hivyo kumwaga mafuta baharini( Picha na Evance Ng’ingo)
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 23rd July 2010 @ 19:16
Wasamaria wema wakisaidia kumuingiza kwenye bajaj dereva wa pikipiki, mkazi wa Dar es Salaam aliyepata ajali baada ya kugongana na gari eneo la Kunduchi, juzi. (Picha na Robert Okanda).
Imetayarishwa na: Imewekwa tarehe: 22nd July 2010 @ 19:12