Hundi na baiskeli
- Post 05 Machi 2013
WAZIRI wa Afya na Ustawi wa jamii Dk Hussein Mwinyi (kushoto) akimpongeza Mwenyekiti wa kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalumu cha Victoria Foundation chenye makao makuu yake mkoani Geita, Vicky Kamata (kulia) baada ya kukabidhiwa hundi yenye thamani ya Sh milioni 10 pamoja na baiskeli 30 kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Sayed Corporation Limited, Sayed Mosood (katikati).
Hafla hiyo ilifanyika juzi jijini Dar es Salaam. (Na Mpigapicha Wetu).

