23Mei2013

 

Waziri- Ujenzi bomba la gesi utaendelea

SERIKALI imewasilisha bungeni hotuba ya bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka ujao wa fedha, huku ikisisitiza kuwa azma ya kujenga bomba la kusafirisha gesi ya asili kutoka Mtwara kuelekea Dar es Salaam iko pale pale.

Soma zaidi...

  • Imeandikwa na Oscar Mbuza, Dodoma
  • Imesomwa mara: 6

Vurugu Mtwara, Kikwete atema cheche

RAIS Jakaya Kiwete amesema serikali itawakamata wanasiasa wanaochochea vurugu mkoani Mtwara kwa kisingizio cha kuzuia gesi isitoke mkoani humo. Rais alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumzia vurugu kubwa zilizotokea Mtwara jana wakati akihutubia wananchi kwenye uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Dodoma - Iringa eneo la Bahiroad. Barabara hiyo ya kilomita 70 ni kutoka Dodoma mpaka Fufu.

Soma zaidi...

  • Imeandikwa na Sifa Lubasi, Dodoma na Waandishi Wetu
  • Imesomwa mara: 51

Uhakiki daftari la wapiga kura kuanza mwezi ujao

TUME ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) imesema itaanza kazi ya kuhakiki daftari la kudumu la wapiga kura mwezi ujao baada ya kupata fedha. Aidha, itafanya tathmini na kuhakiki mipaka ya majimbo ya uchaguzi yaliyopo Unguja na Pemba.

Soma zaidi...

  • Imeandikwa na Khatib Suleiman, Zanzibar
  • Imesomwa mara: 172

Mbunge aambiwa apeleke mawazo yake Tume ya Katiba

MBUNGE wa Kasulu Mjini, Moses Machali (NCCR –Mageuzi) ametakiwa kuwasilisha mawazo yake ya kuanzisha mfumo wa utawala wa majimbo, yatakayoongozwa na magavana kwenye Tume ya Mchakato wa Katiba ili maoni yake yaweze kusikilizwa.

Soma zaidi...

  • Imeandikwa na Sifa Lubasi, Dodoma
  • Imesomwa mara: 143

Maji ya kuwasha watumiayo polisi hayana madhara

NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Perreira Silima amesema, maji ya kuwasha ambayo yamekuwa yakimwagwa na Jeshi la Polisi wakati wa kutawanya watu kwenye vurugu mbalimbali hayana madhara kwa binadamu.

Soma zaidi...

  • Imeandikwa na Sifa Lubasi, Dodoma
  • Imesomwa mara: 149

Wanasiasa wafanya vurugu kukamatwa

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali Said Mwema ameagiza askari kuhakikisha wanawakamata wanasiasa wanaofanya vurugu kwa visingizio vya siasa. Mwema amesisitiza kuwa askari polisi si wanachama wa chama chochote cha siasa, japokuwa wanaruhusiwa kupiga kura.

Soma zaidi...

  • Imeandikwa na Frank Geofray, Jeshi la Polisi
  • Imesomwa mara: 189