23Mei2013

 

Category: Makala

Ngoma ya Wanyambo.

Wanyambo, kabila linalotilia mkazo ustawi wa jamii

WANYAMBO ni kabila dogo katika jamii ya wabantu linalopatikana Kaskazini Magharibi mwa Tanzania katika wilaya za Karagwe mkoani Kagera.

Soma zaidi...

  • Imeandikwa na Kaanaeli Kaale
  • Imesomwa mara: 2

Category: Makala

Baadhi ya wanyama katika Hifadhi ya Ngorongoro.

Kizungumkuti cha utalii je, bajeti imekidhi?

KWA wale wanaofuatilia masuala ya utalii nchini wanaweza kupata ahueni kutokana na hotuba iliyopita ya Waziri wa Maliasili na Utalii katika Bunge la bajeti, hotuba ambayo imeazimia kuipeleka Tanzania katika hatua nyingine ya utalii.

Soma zaidi...

  • Imeandikwa na Beda Msimbe
  • Imesomwa mara: 1

Category: Makala

MAPAMBANO YA UKIMWI-2: Matumizi sahihi ya kondomu yaweza kukuepusha na VVU

KATIKA mfululizo wa makala haya juu ya kukumbushana mambo ya msingi kuhusu Vijidudu Vya Ukimwi (VVU) na Upungufu wa Kinga Mwilini (UKIMWI).

Mwandishi Wetu Bantulaki Bilango leo atachambua matumizi sahihi ya kondomu (za kike na za kiume) na jinsi mtoto anavyoweza kuambukizwa au kuzaliwa bila maambukizo ya VVU wakati wazazi wake wameambukizwa.

PAMOJA na Watanzania wengi kuziona na kuzitumia kondomu, bado matumizi yake kwa walio wengi si sahihi kutokana na ama wengi kuamini wanajua, hivyo hawahitaji ushauri au hawajui kabisa namna ya kuzitumia na wengine, ndio kwanza hawataki hata kuzigusa ingawa wanafanya ngono na wapenzi tofauti tofauti ambao hawajui kama wamepimwa au la.

Kubla ya kuchambua matumizi sahihi ya kondomu, ni vema kuelezea juu ya faida zake. Faida kubwa kwa mtu anayefanya tendo la ngono kwa kutumia kondomu, mbali na kuzuia mimba zisizotarajiwa, inaepusha magojwa mengine mengi ya maambukizi ya magonjwa ya ngono.

Magonjwa haya yamegawanyika katika sehemu kuu mbili: Kundi la kwanza ni magonjwa ya ngono yanayotoa vidonda. Haya ni pamoja na kaswende (cyphilis), pangusa (chancroid), malengelenge na mengineyo. Magonjwa haya yasipodhibitiwa mapema muathirika anaweza kudhurika zaidi kwa kupata madhara kama vile kutoka mimba, kuzaa watoto kabla ya muda wake (njiti), kukatika uume na mengineyo.

Kundi la pili ni magonjwa ya ngono yanayotoa uchafu. Haya ni pamoja na kisonono (Gonorrhea), klamadia (chlamydia), fangasi (genital candidiasis), trakomoniasis na vulva vaginasias. Haya magonjwa hutoa uchafu na mhusika kuwashwa sehemu zake za siri, kusikia maumivu chini ya kitovu na kusikia maumivu wakati wa kujamiiana.

Magonjwa haya yana madhara makubwa kwa mgonjwa ikiwa ni pamoja na kuwa mgumba, mimba kutunga nje ya tumbo la kizazi kwa wanawake huku kwa wanaume wakipata madhara ya kuziba mirija ya mkojo, kuvimba baadhi ya maeneo ya sehemu za siri na utasa.

Pamoja na madhara magonjwa yanaweza kutokea kwa mtu aliyeambukizwa na magonjwa ya zinaa, kubwa zaidi anakuwa katika hatari ya kuambukizwa VVU ikilinganishwa na yule ambaye hana magonjwa haya.

Hivyo ni vema kutumia kondomu, tena kwa usahihi kama moja ya njia ya kujikinga na maradhi lakini hasa hasa ugonjwa huu Ukimwi ambao hauna kinga wala tiba. Katika matumizi ya kondomu, ni lazima watumiaji wakubaliane kwa kuwa zipo za aina mbili; za kike na za kiume na zote haziwezi kutumika kwa wakati mmoja.

Mtaalamu wa Afya ambaye pia ni Mkufunzi katika Chuo cha Afya Tanga, Lucas Munaku anasema wawili wanapoamua kutumia kondomu ni lazima wakubaliane kwa kuwa mali ghafi zilizotengeneza kondomu za kike na za kiume ni tofauti, hivyo ni vema kukawepo makubaliano ya nani avae na nani asivae na sio kuvaa wote kwa pamoja au kutovaa kabisa.

Munaku anasema kwa kuvaa wote wawili, katika msuguano wakati wa tendo, kunaweza kusababisha kupasuka kwa kundomu hizo hivyo kufanya tendo hilo kufanyika bila kinga.

Matumizi ya kondomu kwa wanaume

Mtumiaji wa kiume, kwanza ni lazima aikague kabla ya kuamua kuitumia ili aone kama iko katika hali nzuri ya matumizi. Haishauriwi kutumia kondomu iliyokwisha muda wake, hivyo mtumiaji ni lazima aangalie muda wa kutengenezwa na ule wa kuisha. Haitumiki zaidi ya mara moja. Hata hivyo, inashauriwa pia zilizo katika matumizi bora zaidi ni zile ambazo hazijapitisha muda wa miaka miwili tangu zitengenezwe.

Mtumiaji mwanamume ni lazima baada ya kuhakikisha muda wake na kujiridhisha, achukie ile pakiti ya kondomu na kuangalia kama bado ina hewa, kama haina, pakiti hiyo imeharibika na si salama. Wakati wa kuichana, ni lazima iangaliwe sehemu yenye misumeno ya pakiti kwa uangalifu, ichanwe bila kuharibu kondomu yenyewe iliyoko ndani, iminywe ili itokeze katika eneo lililochanwa.

Na hakikisha tendo la kuvalisha kondomu hiyo mwanamume yuko tayari kwa tendo la ngono na si vinginevyo. Wakati wa kuvaa, ni lazima mkunjo wake, uwe nje na ikitokea ukawa ndani ikagundulika wakati wa kuivaa, ni vema ikatumika nyingine kwa kuwa tayari itakuwa imeharibiwa. Ikidondoka chini itupwe badala ya kuiokota na kuitumia.

Jambo jingine la kuzingatia ni kuhakikisha wakati inavaliwa haina hewa au mpasuko wowote, vinginevyo itakuwa kazi bure. Baada ya tendo la ngono, kondomu ivuliwe haraka wakati mambo bado yako sawa na mwanamke anaweza kusaidia kuitoa kwa uangalifu bila kuruhusu mbegu za kiume kumwagika na baadaye itumbukizwe kwenye choo cha shimo.

Katika mfululizo wa makala haya, Jumatatu tutazumgumzia matumizi ya kondomu ya kike, mate kama yanaambukiza ama la na maambukizo kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Kama nafasi itaruhusu tutaangalia pia unyanyapaa na sababu za wanawake kuambukizwa zaidi kulinganisha na wanaume.

  • Imeandikwa na Bantulaki Bilango
  • Imesomwa mara: 6

Category: Makala

Wanafunzi kama hawa wa mkoani Katavi watafaidika na uboreshaji wa ufundishaji wa Kingereza katika shule za msingi na sekondari.

Uingereza yajitosa kuokoa Kingereza mashuleni

MATATIZO ya kielimu yanachangiwa na mambo mengi, mojawapo linalowagusa wanafunzi moja kwa moja kutokukielewa vizuri Kingereza ambacho wanakitumia kama lugha maalumu ya mawasiliano kwa mana ya kujifunzia katika masomo ya sekondari, kuuliza maswali ili kuelewa zaidi na kujibia mtihani.

Soma zaidi...

  • Imeandikwa na Shadrack Sagati
  • Imesomwa mara: 144

Category: Makala

Wajumbe wa Mkutano wa Kimataifa wa Wataalamu wa Maji barani Afrika (AfWA) wakisikiliza mada. Mkutano huo uliofanyika Dar es Salaam wiki iliyopita, uliambatana na maonesho ya bidhaa na huduma za sekta ya majisafi na majitaka.

Wataalamu wakuna vichwa kukomesha upotevu wa maji

“NCHI nyingi zina matatizo ya maji. Hakuna mji katika bara la Afrika usiokuwa na tatizo la maji. Uvunaji wa maji ya mvua utakuwa suluhisho. Hata Dar es Salaam ambako kuna Bahari ya Hindi, bado kuna tatizo kubwa la maji, kwa sababu maji yake ni ya chumvi na teknolojia ya kuyabadilisha haipo.”

Soma zaidi...

  • Imeandikwa na Nelson Goima
  • Imesomwa mara: 45

Category: Makala

Kutoka kushoto, Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, Rais Jakaya Kikwete na Rais Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa. Wote katika awamu zao wamepambana na Ukimwi.

MAPAMBANO YA UKIMWI-1: Tukabili VVU na Ukimwi kwa kupima, kubadili tabia

ELIMU ya Virusi Vya Ukimwi (VVU) na Upungufu wa Kinga Mwilini (Ukimwi) imeenea kila kona ya nchi na duniani kote.

Soma zaidi...

  • Imeandikwa na Bantulaki Bilango
  • Imesomwa mara: 51