EWURA Banner
HabariLeo Logo
 
Tafuta:
 
 
 
Makala

Kikwete: Soko la maziwa lipo changamkieni kufuga ng’ombe
Imeandikwa na Na Magnus Mahenge; Tarehe: 8th November 2009 @ 23:59 Imesomwa na watu: 1044; Jumla ya maoni: 1


Image

Habari Zaidi:
  • ‘Kiswanglish’ kinaharibu vijana
  • Faida za ubunifu wa biashara ya maua makavu
  • Vitabu vya Marekani kuinua elimu ya sayansi nchini
  • Tishio la ongezeko la Ukimwi Mara
  • Changamoto za sekta binafsi za ulinzi Tanzania.East African Security: Tunazikwa kimya kimya
  • Wakulima Morogoro wachanga fedha wanufaika na masoko ya kisasa
  • Ziara za Marekani za Rais Kikwete zazaa matunda
  • Sheria mpya ya mbolea kukabiliana na udanganyifu wa pembejeo.
  • Dk Shein: Nitajenga umoja wa Wazanzibari
  • Tusipotoshe watu kuwa kura zinaibwa
  • Slaa acha kujilinganisha na Rais Kikwete
  • Rombo yahitaji mbunge mwenye mapya
  • Maisha ya wachezaji soka yalivyo hatarini
  • AY katika safari ya kuitangaza Bongofleva Ufaransa
  • ABUNU RAMADHANI:Mkali wa soka anayemuota Maximo
  • GABRIEL KULIGI:Mkali wa karate, kick boxing Kanda ya Ziwa
  • Sido yawapiga jeki waganga wa jadi
  • Umuhimu na Utajiri wa Bonde la Rufiji
  • Historia ya utamaduni wa majengo ya kale
  • Maabara za meza kuwakomboa wanafunzi Dar es Salaam

  • Habari zinazosomwa zaidi:
  • Balaa lingine kwa Chenge
  • Salama: Jasiri aliyetangaza kuishi na virusi vya Ukimwi
  • Dina Marius, mrithi wa Amina Chifupa
  • ‘Housigeli’ anataka kuniharibia ndoa
  • Vatican yamvua jimbo Askofu
  • Kikwete achekecha wakuu wa wilaya
  • Waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano waongezeka kwa 22%
  • Interpol yatumika kusaka wenye zeutamu
  • Orijino Komedi, Jay Dee waitwa Iringa
  • JK apigilia msumari wa mwisho Dowans
  • HAKUNA jambo jema kama mfugaji wa ng’ombe kuhakikishiwa soko la bidhaa kama maziwa ambayo ikikaa muda mrefu inaharibika.

    Wafugaji wa mjini Njombe mkoani Iringa pamoja na vitongoji vinavyozunguka, wameahidiwa soko la uhakika na Kiwanda cha Kusindika maziwa kilichojengwa mjini humo.

    Rais Jakaya Kikwete alipotembelea kiwanda hicho Oktoba 28, mwaka huu, kinachozalisha na kufanya biashara ya mazao ya maziwa wilayani Njombe, akasikia kuwa kiwanda kina uwezo wa kusindika zaidi ya lita 4,000, lakini kwa sasa kinapokea maziwa lita 2,200.

    Kiwanda kinasindika chini ya uwezo wake kwa lita 1,800, ndiyo maana akawahimiza wananchi wa wilaya ya Njombe, kuchangamkia nafasi ya kufuga ng’ombe wengi wa maziwa, kwani tayari kiwanda hicho kimewatengenezea soko la uhakika la maziwa wanayokamua kutoka kwenye ng’ombe wao.

    Akisoma taarifa ya utendaji wa mradi wa kiwanda hicho, uliobuniwa na wadau wa maendeleo ya ufugaji katika wilaya ya Njombe, mbele ya Rais Kikwete, Meneja Mradi, Edwin Kidehele, anasema kiwanda hicho kinafanya kazi chini ya uwezo wake kwa asilimia 45 kwa siku moja.

    “Kiwanda hiki kina uwezo wa kupokea lita 4,000 za maziwa kwa siku, kwa sasa kiwanda kinapokea lita 2,200 kwa siku, maziwa ambayo ni sawa na asilimia 55 ya uwezo wa kiwanda hicho kwa siku,” alisema Kidehele.

    Kwa kubaini fursa kubwa ya wananchi wilayani humo kwenye kiwanda hicho, Rais Kikwete amewataka watumie nafasi hiyo ya soko la uhakika kwa kufuga ng’ombe wengi zaidi ili kupata maziwa na kuuza kiwandani.

    Wananchi wanatakiwa kufuga ng’ombe kwa wingi na kuzalisha maziwa na kutumia fursa ya usafiri wa kiwanda unaopita katika maeneo wanayofuga vijijini na kukusanya maziwa na kuyafikisha kiwandani na baadaye mengine kuyasambaza katika shule.

    Rais Kikwete amewahimiza wana-Njombe kutumia uwepo wa kiwanda hicho kutokana na ukweli kuwa kiwanda kinapokea maziwa kidogo, ambayo pia yanachangia mapato ya kiwanda kuwa kidogo.

    Kiwanda kinapata wastani wa Sh milioni 42 kwa mwezi ambazo ni sawa na asilimia 45 ya uwezo wa kiwanda, kumbe ingewezekana kupata zaidi kama kiwanda kingepokea maziwa mengi zaidi.

    Kiwanda kinazalisha chini ya kiwango hata kama kina mashine na mitambo ya kisasa ambayo imefungwa hivi karibuni kwa ajili ya kusindika na kufanya lita 600 za yoghurt kwa siku.

    Kiwanda hicho kimekuwa mkombozi kwa wafugaji 521 ambao wana jumla ya ng’ombe 2,724 wanaotoa maziwa na hivyo kukusanywa na kiwanda hicho kutoka kwenye mashamba yao na kufikisha kiwandani kutengeneza bidhaa mbalimbali.

    Kuanzishwa kwa mradi wa kiwanda hicho, mmoja wa wafugaji Athanas Kidenye anasema, umekuwa chimbuko la ajira kwa watu mbalimbali huko mashambani kwetu, kuanzia wakata nyasi, wakamuaji maziwa, wafugaji na wachungaji, wauzaji maziwa na wasombaji maziwa kutoka mashambani hadi kwenye vituo na kiwandani.

    Bidhaa zinazotengenezwa na kiwanda hicho ni pamoja na maziwa yaliyogandishwa, yoghurt na jibini, bidhaa ambazo zina soko la uhakika wilayani Njombe kwa ujumla, pia katika eneo la Makambako, Iringa, Mbeya, Songea, Morogoro na Dar es Salaam.

    Kidehele anasema wakati wafugaji wakineemeka kwa kupata soko la uhakika, wanafunzi nao wanaandaliwa mazingira mazuri ya kupata lishe ya maziwa wakiwa shuleni huko huko, kupitia ‘Mpango wa Kunywesha Maziwa Shuleni.’

    Mpango wa kunywesha wanafunzi maziwa shuleni, utazihusisha shule 28 za msingi kati ya shule 75 za wilaya hiyo, hivyo utahusisha wanafunzi zaidi ya 5,000 kwa wiki, ambao watapata lishe kamili ili wasome masomo vizuri.

    Ukusanyaji maziwa vituoni kwa kutumia gari la kiwanda na unyweshaji maziwa shuleni, unazingatia ubora wa maziwa. Maziwa yanayochukuliwa ni salama baada ya kuwa ng’ombe wamepimwa kama wana maradhi.

    Upimaji huo unafanyika kwa ushirikiano na Kamati ya Ulaya ya Mafunzo na Kilimo, Cefa Italia, Njolifa, Kituo cha Upimaji Mifugo Iringa na wataalamu wa kilimo na mifugo wa halmashauri ya mji na wilaya ya Njombe.

    Kiwanda kimekuwa makini kutopokea maziwa ambayo ng’ombe wake hawajapimwa, ndio maana katika kipindi cha mwaka 2008/09, kiwanda kilifaulu kupima ng’ombe 2,724 ambao ni sawa na asilimia 81.72 ya lengo na ndio ng’ombe ambao maziwa yao yalipokelewa.

    Kiwanda kimekuwa kikitoa mafunzo kwa wafugaji na kupima ng’ombe dhidi ya magonjwa kama kifua kikuu na Brucellosis, lakini pia kimekuwa kikitoa semina na mafunzo ya ufugaji bora wa ng'ombe wa maziwa kwa wafugaji na kuangalia usafi wa maziwa na umuhimu wa kunywa maziwa hayo.

    Kidehele anasema, mafunzo hayo yanalenga pia kupunguza vifo vya ng’ombe wa maziwa vinavyoenezwa na magonjwa ya kupe kwa asilimia 75, lakini pia mafunzo hayo yanalenga kuhamasisha wafugaji kuwa na walau ekari nne za shamba la malisho bora ya mifugo yao.

    Lakini pia wafugaji wanapata elimu ya kuboresha ubora wa bidhaa na vifungashio kwenye chupa za maziwa, ya kupanua uwigo wa masoko ya maziwa na kupata wateja wengi zaidi wa bidhaa hiyo.

    Mafunzo hayo yanalenga kuongeza ushirikiano na mshikamano zaidi baina ya wafugaji, kamati za shule, maofisa mifugo na Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) ili kuongeza ubora wa huduma za kiwanda na masoko ya ndani na nje.

    Kiwanda hicho ambacho kimeanzishwa na wadau kadhaa wakiwamo Umoja wa Wakulima na Wafugaji wa Ng’ombe Njombe (Njolifa), Kanisa Katoliki Njombe, Halmashauri ya Mji wa Njombe na Cefa ambalo ndio wahisani na wasimamizi wa mradi huu.

    Mradi wa kiwanda hicho, uliobuniwa na wadau hao wa wa maendeleo ya mifugo katika wilaya hiyo, baada ya kujifunza na kuona jitihada za mashirika mengine ya wahisani yanavyoendeleza wafugaji katika maeneo mengine.

    Mashirika ambayo yalikuwa kichocheo cha wafugaji wa Njombe kuanzisha miradi huo ni wamisionari, makanisa, watu binafsi pamoja na serikali lakini pia walishawishika baada ya kuona Mradi wa Maendeleo ya Ng’ombe wa Maziwa Nyanda za Juu Kusini (SHDDP) na Mradi wa Kimataifa wa Ufugaji Mitamba (HPIT).

    Meneja huyo anasema, taasisi zote hizo zilizojiingiza katika ufugaji wa ng’ombe wa maziwa wilayani Njombe chini ya idara ya kilimo na mifugo, zilikuwa kichocheo kikubwa kwa Njolifa kuanzisha mradi huo.

    Taasisi hizo hasa za kimataifa, zilianza kazi ya kuwawezesha wafugaji wa ng’ombe wa maziwa wilayani ambao kwa kufuga huko walichangia pato la wafugaji wenyewe, lakini pia walipata changamoto ya kuongeza matimizi ya maziwa kama lishe.

    Kuwezeshwa wafugaji hakukutosha, ilihitajika kianzishwe chombo cha kuendeleza na kuimarisha ufugaji wa ng’ombe wa maziwa ili uchangie ipasavyo katika pato la wafugaji wenyewe ndipo Njolifa ikazaliwa.

    Njolifa haikusimama peke yake, Kanisa Katoliki kwa upande wake, kwa miaka mingi walikuwa wakisaidia kuelimisha na kuhimiza matumizi ya mifugo na mazao yake katika parokia na vituo vyake.

    Kanisa Katoliki kwa upande mwingine, ndilo lililokuwa mhamasishaji namba moja na mhusishaji wa shirika la wahisani kutoka Italia, Cefa, kushiriki, kubuni na kupanga maandalizi ya mradi huo ulibadilisha maisha ya wafugaji wa Njombe kwa kuwa na uhakika wa soko la maziwa yao.

    Katika mchakato huo wa kuhamasisha wananchi kufuga ng’ombe kwa wingi, halmashauri ya mji na wilaya ya Njombe, walikuwa mhimili mkubwa katika kutoa elimu kwa wananchi kupitia maofisa ugani wa mifugo na ndio walikuwa wasimamiaji wa sera ya mifugo katika kutekeleza mradi huo.

    Licha ya mafanikio hayo, Meneja mradi wa kiwanda hicho Kidehele anasema, mradi huo unakabiliwa na changamoto mbili, moja ni kuwa na gari moja tu la kusomba maziwa, lakini la pili ni gharama za pembejeo za ng’ombe wa maziwa kama dawa za kupimia kifua kikuu na Brucellosis, dawa ya kutibu magonjwa yanayoenezwa na kupe, zinakatisha tamaa wafugaji kuendelea kufuga ng’ombe wa maziwa.

    Changamoto hiyo, inakwamisha maendeleo ya mifugo ambayo Rais Kikwete katika ziara yake mkoani Iringa, Oktoba 26 hadi 29, mwaka huu, ameamua kuweka msukumo katika kuangalia sekta ya mifugo baada ya kuridhishwa na maendeleo ya utekelezaji wa Kilimo Kwanza.

    Sekta ya mifugo pamoja na mazao yake itafikia kiwango cha kuwa maarufu kama ‘Kilimo Kwanza’ kama serikali itatupia macho suala la kuweka ruzuku kwenye dawa za mifugo kama ilivyoweka kwenye mazao ya kilimo, jambo ambalo litachangia katika kulinda afya za watumiahi wa maziwa na bidhaa zake ili kuongeza uzalishaji.

     
         
     
    Jumla Maoni (1)
         
    Maoni   Hongera sana Njombe Mungu awabaki sana Nesphori Kaza buti.
         
     
     
      Tuma Maoni yako
       

    Jina la Kwanza:

    Jina la mwisho:
    Baruapepe: Barua Pepe imekosewa.
    Maoni yako:   Andika Maoni yako tafadhali.Tafadhali andika Maoni yako.
     
     
     
    WAZO LANGU
    Image

    Magereza fanyieni kazi malalamiko ya wafungwa

    SOMA | HIFADHI
    SAFU
    Image

    Tekuteku za Tefutefu!

    SOMA | HIFADHI
    NYOTA WA WIKI
    Image

    Mtangazaji kajikomboa kwa kuanzisha redio

    SOMA | HIFADHI
    JISAJILI NASI
    Jina la kwanza:
    Jina la Ukoo:
    Baruapepe: A value is required.
     
     
     
    Wasiliana nasi mhariri@habarileo.co.tz, advertising@dailynews.co.tz
    Simu:+255 22 2 127492 au 22 2 116074 au +255 22 2 110595 au 22 2 127493
    HabariLeo © 2009 Haki zote zimehifadhiwa.
    DailyNews Building, Plot 7, Samora Avenue, Box 9033, Dar es Salaam, Tanzania Copyright © 2009 DailyNews Media Group
    Advertisement
    TSN Adveritising